Joy FM

ALAT Kigoma yatembelea miradi ya maendeleo Kibondo

15 August 2026, 11:46

Wajumbe wa ALAT wakiwa kwenye picha na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya Kibondo, Picha na Mwandishi wetu

Halmashauri ya Wilaya Kibondo Mkoani Kigoma imepongezwa kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi

Na Mwandishi wetu

‎Wajumbe wa jumuiya ya tawala za Mitaa Tanzania,  ALAT Mkoa wa Kigoma wametakiwa kuendelea kishirikiana katika kufikia malengo ya kukuza maendeleo na uchumi wa halmashari za mkoa wa Kigoma.

Muonekano wa mradi wa ofisi za Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Kibondo, Picha na Mwandishi wetu

Mwenyekiti wa ALAT mkoa wa Kigoma Bw. Alex Baragomwa amesema hayo wakati wa kikao cha jumuia hiyo  cha kujadili na kupitia taarifa za robo ya nne ya mwaka wa fedha 2025/2026, kikao ambacho kimefanyika wilayani Kibondo

‎Baragomwa amesema ushirikiano wa wajumbe utasaidia kuinua uchumi wa halmashauri zote 8 za mkoa huo

‎Kabla ya kikao hicho, ALAT Mkoa wa Kigoma imeanza na ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa wilayani Kibondo ambayo ni chuo cha maafisa tabibu, Soko jipya la kisasa la Nane nane, Jengo la halmashauri, vibanda vya soko la samaki pamoja na kikundi cha wajasiliamali cha Kaa kazi.

Muonekano wa mradi wa ofisi za Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Kibondo, Picha na Mwandishi wetu

‎‎Hata hivyo wajumbe wa ALAT wameipongeza halmashauri ya wilaya ya Kibondo kwa ushirikiano ambao unafanyika katika kutekeleza miradi ya maendeleo

Mkuu wa wilaya ya Kibondo Kanali mstaafu Aggrey Magwaza pamoja na Mweyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Wilaya ya Kibondo Bw. Hamisi Tahiro wameipongeza jumuia ya ALAT kwa kuendelea kuimarisha ufuatiliaji wa shughuli za maendeleo ndani ya mkoa wa Kigoma.