Joy FM

Vikundi 30 vyanufaika na mikopo ya milioni 300 Kigoma

9 June 2026, 11:22

Wanufaika wa mikopo ya asilimia kumi wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wakati wa zoezi la utoaji wa mikopo hiyo, Picha na Lucas Hoha

Mikopo hiyo inayotolewa na Benki ya CRDB ambayo inatokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ni moja ya njia muhimu za kuwawezesha wananchi wenye kipato cha kujikwamua kiuchumi na mikopo hii imeanzishwa kwa lengo la kuwapa wanufaika mtaji wa kuanzisha au kuendeleza shughuli mbalimbali za uzalishaji mali na hivyo kuboresha maisha yao na ya familia zao

Na Lucas Hoha

Wanufaika wa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 300 katika Manispaa ya Kigoma Ujiji wametakiwa kutumia fedha hizo kwa bidii, weledi wa ujasiriamali na usimamizi mzuri wa biashara zao ili kuhakikisha wanarejesha mikopo hiyo kwa wakati na kuepuka hatua za kisheria zitakazoweza kuchukuliwa dhidi yao.

Taarifa na Lucas Hoha.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ambaye pia ni Afisa Elimu Sekondari wa manispaa hiyo, Kajanja Lawi, wakati akifungua mafunzo kwa vikundi 30 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vilivyonufaika na mikopo hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ambaye pia ni Afisa Elimu Sekondari wa manispaa hiyo, Kajanja Lawi

Kwa upande wake, Afisa Maendeleo wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Jabir Majira, amesema manispaa hiyo inaendelea kutekeleza sera, kanuni na miongozo ya Serikali kwa kuhakikisha mikopo hiyo inatolewa kwa wakati, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwawezesha wananchi kiuchumi na kupunguza umasikini.

Sauti ya Afisa Maendeleo wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Jabir Majira

Nao baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuweka mazingira wezeshi ya upatikanaji wa mikopo kwa wajasiriamali, wakisema hatua hiyo imewasaidia kuongeza uzalishaji na kuendesha shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi zaidi.

Sauti ya baadhi ya wanufaika wa mikopo

Mikopo hiyo imetolewa kwa vikundi mbalimbali vya wajasiriamali katika Manispaa ya Kigoma Ujiji kupitia Benki ya CRDB Tawi la Kigoma, kwa mujibu wa maelekezo na miongozo ya Serikali.