Joy FM

 Vikundi 13 vya watu wenye ulemavu vyapatiwa mikopo Kakonko

29 April 2026, 12:11

Baadhi ya wanavikundi vya watu wenye ulemavu vyapatiwa mikopo, Picha na Mwandishi wetu

Vikundi 13 vya walemavu vimepatiwa mkopo kati ya vikundi 23 ambavyo vimepatiwa mkopo wa halmashauri ya wilaya ya Kakonko katika robo ya pili ya mwaka wa fedha wa 2025/2026

Mkopo huo umetolewa ikiwa ni mkakati wa serikali wa kuviwezesha vikundi vya walemavu kati ya vikundi vya wanawake na vijana ambapo vikundi hivyo vimepata milioni 51 kati ya milioni 106 zilizotolewa.

Baadhi ya wanavikundi vya watu wenye ulemavu vyapatiwa mikopo, Picha na Mwandishi wetu

Afisa maendeleo ya jamii halmashauri ya wilaya ya Kakonko Bw. Mustapha Mtungwe amesema vikundi vingine ambavyo vimepatiwa mkopo ni vikundi 10 vya wanawake na vijana na mkopo huo ukawe chachu ya kukuza uchumi.

Sauti ya Mustapha Mtungwe, afisa maendeleo Kakonko
Ustapha Mtungwe, afisa maendeleo Kakonko, Picha na Mwandishi wetu

Naye mratibu wa mikopo idara ya maendeleo ya jamii halmashauri ya wilaya ya Kakonko Bi. Safia Mjuberi amewataka wanavikundi  kutekeleza miradi yao kulingana na malengo ambayo walijiwekea wakati wa kuomba mkopo