Joy FM
Joy FM
16 April 2026, 4:52 pm

Shule ambayo haina madirisha, mapazia bado yanaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya kujifunzia kwani yanaweza kuwa na umuhimu hata kwa shule ambayo haina madirisha, ingawa mara nyingi huonekana kama yanahitajika zaidi kwenye madirisha.
Na Michael Mpunije
Umoja wa Wananchi wa kata ya Mwayaya wanaoishi katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam wametoa msaada wa pazia 24 zenye thamani ya shilingi laki tano (500,000) kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Manyovu, iliyopo Kata ya Mwayaya, Wilayani Buhigwe Mkoani kigoma
Msaada huo umetolewa ili kusaidia kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa madirisha katika baadhi ya vyumba wanavyotumia wanafunzi wanaoishi bweni shuleni hapo, hali ambayo imekuwa ikiathiri mazingira yao ya kujifunzia na kuishi.
Akikabidhi vitu hivyo kwa niaba ya wanamwayaya waishio mikoa ya pwani na Dar es salaam Diwani wa kata ya mwayaya Ephraim Sibanganya mwakeye ameeleza kuwa lengo la msaada huo ni kuboresha ustawi wa wanafunzi na kuwapatia mazingira bora zaidi ya kujifunzia huku akiwasisitiza kuongeza bidii katika masomo.

Awali, Mkuu wa Shule ya Sekondari Manyovu, Mwalimu Najimu ahmad mpendq alieleza kuwa shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa madirisha katika vyumba vya wanafunzi wanaoishi bweni, hali inayosababisha ukosefu wa faragha kwa wanafunzi ambapo licha ya jitihada mbalimbali zinazofanywa na uongozi wa shule, bado kuna uhitaji mkubwa wa maboresho ya miundombinu ili kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira salama na rafiki kwa ajili ya kujifunza na kuishi.
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Manyovu wameushukuru Umoja wa wana Mwayaya kwa msaada wa pazia walioutoa.
Wakisema kuwa msaada huo umesaidia kuboresha mazingira ya malazi shuleni hapo, hasa kwa kuwakinga na upepo na baridi kali na kuwapatia faragha wakiwa vyumbani, hali itakayowawezesha kusoma kwa utulivu zaidi na kuongeza umakini katika masomo yao.