Joy FM

Madiwani watakiwa kutoa taarifa za miradi ya maendeleo kwa wananchi Kasulu

30 July 2026, 12:39

Madiwani wa halimashauri ya wilaya ya kasulu katika kikao cha mwisho cha baraza, Picha na Emmanuel Kamangu

Katibu tawa wa Wilaya Kasulu Bi. Teresia Mtewele amwataka madiwani kuhakikisha wanatoa taarifa za miradi ya maendeleo inayotelelezwa kwenye maeneo yao ili wananchi waweze kuifahamu

Na Emmanuel Kamangu

Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu wametakiwa kuhakikisha wanajitahidi kutoa mrejesho kwa wananchi juu ya  shuguli mbali mbali za maendeleo zinazotekelezwa na serikali ya awamu ya sita.

Amebainisha hayo katibu tawala wilaya ya kasulu Bi Teresia Mtewele kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Kasulu  Kanal Isack Mwakisu katika kikao baraza la madiwan  cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2025/26 ambapo amewasihi madiwani kujenga utaratibu wa kuzungumza na wananchi ili kutambua kazi nzuri za maendeleo zinazoendelea kufanywa na serikali katika kata zao.

Katibu tawala wa wilaya ya kasulu Bi Tereseia Tewele katika kikao cha mwisho cha baraza la Madiwani katika halmashauri ya wilaya ya kasulu, Picha na Emmanuel Kamangu

Aidha  Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu Bw, Benjamini Charles amewataka madiwani wenzake kuendelea kushirikiana na wananchi kikamilifu katika kuhakikisha wanawaletea maedndeleo.

Kwa upande wao baadhi ya madiwani mmoja wao akiwa Bw, Edson Hanyuma wameipongeza serikali ya awamu ya sita kwanamuna inavyoendelea kutekeleza maendeleo katika kata mbali mbali za wilaya hiyo jambo linaloakisi utendaji kazi wa raisi Dkt samia Suruhu hasani katika kuwaletea wananchi maendeleo.

 Kikao hiki cha mwisho cha baraza la madiwani kwa mwaka wa fedha 2025/26 kimetanguliwa na  baraza taarifa  za kila kata na kufuatiwa na baraza la Madiwani ikiwa ni sehemu ya kujadili shuguli mbali mbali  za maedneleo zinazotekelezwa na serikali ndani ya halmashauri ya wilaya ya kasulu.

Sauti ya Mwandishi we Emmanuel Kamangu