Joy FM

Viongozi wa dini watakiwa kuwa waadilifu na kumtegemea mungu

3 March 2025, 15:15

Askofu mkuu wa Kanisa la FPCT Tanzania askofu Steven Mulenga, Picha na Hagai Ruygaila

Askofu Mkuu wa Kanisa la FPCT Tanzania amesema viongozi wa dini hawana budi kusimama imara na kuwa waadilifu katika kuwatumikia waumini wao.

Na Hagai Ruyagila

Viongozi wa dini katika Kanisa la FPCT Jimbo la Kasulu mkoani Kigoma wametakiwa kuwa waadilifu kwa kumtegemea Mungu ili kuwa kioo katika jamii inayowazunguka.

Ni katika ibada maalumu ya Kanisa la FPCT Kasulu Mjini ibada ambayo imeongozwa na Askofu mkuu wa kanisa la FPCT Tanzania Askofu Steven Mulenga wakati wa kusimika viongozi mbalimbali wa Jimbo la Kasulu.

Baadhi ya waumini wa kanisa la FPCT, Picha na Hagai Ruyagila

Askofu Mulenga amesema kiongozi wa dini unatakiwa kuwa mfano wa kuigwa na katika kazi unayoifanya sambamba na kuepuka mafundisho ya mitandaoni badala yake kumshirikisha Mungu katika maandalizi ya Neno la Mungu kwa ajili ya kuiweka jamii pamoja.

Sauti ya Kanisa la FPCT Kasulu Mjini ibada ambayo imeongozwa na Askofu mkuu wa kanisa la FPCT Tanzania Askofu Steven Mulenga

Kwa upande wake, Mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Kasulu Sabato Kigongo amewaomba viongozi wa dini kuendelea kuilinda amani tunapoelekea katika uchaguzi mkuu wa viongozi wa serikali ifikapo mwezi oktoba mwaka huu.

Sauti ya Mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Kasulu Sabato Kigongo
Mwakilishi wa Mkuu wa wilaya ya Kasulu Sabato Kigongo, Picha na Hagai Ruyagila

Naye Askofu wa jimbo la Kasulu Shedrack Bunono amesema kama   viongozi waliochaguliwa wanahitaji ushirikiano mkubwa kutoka kwa waumini ili kuongeza maendeleo zaidi waweze kuendelea kuihubiri injili ambayo itawasaidia watu kumjua Mungu sanjari na kubadili maisha yao yaweze kumpendeza Mungu.

Sauti ya Naye Askofu wa jimbo la Kasulu Shedrack Bunono