Joy FM

Madereva pikipiki watoa msaada kwa wagonjwa Kasulu

21 July 2026, 09:25

Afisa wa Polisi Kasulu akikabidha moja ya vitu vilivyotolewa na bodaboda kama msaada kwa wagonjwa Hospitali ya Mlimani Kasulu. Picha na Hagai Ruyagila

Kutoa misaada kwa wagonjwa waliolazwa hospitalini ni kitendo cha huruma, upendo na mshikamano kinachochangia kuboresha ustawi wa wagonjwa na familia zao na misaada hiyo inaweza kujumuisha vyakula, sabuni, nguo, vifaa vya usafi na mahitaji mengine muhimu yanayosaidia kurahisisha maisha ya wagonjwa wakati wa matibabu.

Na Hagai Ruyagila

Maafisa usafirishaji (bodaboda) katika stendi kuu ya mabasi Kasulu mjini wametoa msaada wa vitu mbalimbali, kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi ya watoto Hospitali ya Mlimani, Halmashauri ya Mji Kasulu mkoani Kigoma.

Mwenyekiti wa bodaboda kijiwe cha stendi mpya akitoa msaada. Picha na Hagai Ruyagila

Akizungumza wakati wa kukabidhi Msaada huo Bakari Miraji Rashidi Mwenyekiti wa maafisa usafirishaji hao amesema wataendelea kutoa msaada kwa wahitaji mbalimbali ili kuwapa faraja na kuwatia moyo.

Sauti ya Mwenyekiti wa bodaboda

Mkuu wa usalama barabarani wilaya ya Kasulu, Mrakibu wa polisi Patrick Damas, amewapongeza waendesha bodaboda hao kwa wazo lao la kuwajali wagonjwa, akieleza kuwa kitendo hicho ni mfano mzuri unaopaswa kuigwa na makundi mengine katika jamii.

Sauti ya Patrick Damas
Mkuu wa usalama barabarani wilaya ya Kasulu, mrakibu wa Polisi Patrick Damas. Picha na Hagai Ruyagila

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi na Polisi Kata wa Nyamnyusi, Willy Lupa, amewataka maafisa usafirishaji hao kuendelea kudumisha amani, upendo na mshikamano.

Sauti ya Willy Lupa
Mkaguzi msaidizi wa Polisi na Polisi Kata wa Nyamnyusi Willy Lupa. Picha na Hagai Ruyagila

Kaimu Muuguzi mfawidhi hospital ya Mlimani halmashauri ya Mji kasulu Magreth Nyamuhanga ameeleza namna walivyopokea msaada huo kwa ajili ya wagonjwa.

Sauti ya Magreth Nyamuhanga
Kaimu Muuguzi mfawidhi hospital ya mlimani halmashauri ya Mji Kasulu Magreth Nyamuhanga. Picha na Hagai Ruyagila

Baadhi ya wazazi wa watoto waliopokea msaada huo wametoa shukrani kwa maafisa usafirishaji hao amaarufu bodaboda kwa moyo wao wa kujitolea, huku wakisema utawasaidia kutatua baadhi ya changamoto mbalimbali.

Sauti ya Wagonjwa
Katika picha ya pamoja ni baadhi ya madereva bodaboda na viongozi wa Jeshi la Polisi Kasulu. Picha na Hagai Ruyagila