Joy FM
Joy FM
22 April 2026, 16:17

Msaada huu si tu wa kuokoa maisha kwa muda mfupi, bali pia kuwasaidia waathiriwa kujijenga upya na kuwa na uwezo wa kujitegemea tena
Na Mwandishi wetu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa pole kwa wananchi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji waliopoteza makazi yao baada ya kukumbwa na mafuriko kufuatia mvua kubwa na kusababisha nyumba zao kubomoka.
Pole hizo za Rais Samia zimetolewa kwa niaba yake na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, wakati wa kugawa misaada ya mahitaji muhimu kwa wananchi waliopatwa na kadhia hiyo kutoka katika kata sita kati ya kata 19 za Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Balozi Sirro amesema ni wajibu wa serikali kuhakikisha kwamba inazuia hali kama hiyo kuendelea kutokea kwa siku zijazo ikiwemo kuchukua hatua za kuimarisha miundombu.
Aidha misaada iliyotolewa ni pamoja na unga wa Sembe kilo 1,000, Mchele kilo 1,200, Maharage kilo 800, Sukari kilo 200 Mafuta lita 400 na Sabuni kilo 120, ambapo Balozi Sirro amesema misaada iliyotolewa imewalenga wale waliopata madhara makubwa zaidi.
Hata hivyo baadhi ya wathirika wa mafuriko hayo wameshukuru kwa msaada huo huku wakiomba serikali kukarabati barabara na maneo yote yalioathirika na mvua hizo.
