Joy FM
Joy FM
15 April 2026, 1:10 pm

Ziara ya Kamati ya Uchumi inaelezwa kuwa ni hatua muhimu katika kuhakikisha miradi ya kimkakati inaleta matokeo chanya, ikiwemo kuongeza ajira, kukuza uchumi wa ndani, na kuboresha maisha ya wananchi.
Na Mwandishi wetu
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, elimu na afya Manispaa ya Kigoma Ujiji Mhe. Gregory Keberezo ameongoza wajumbe wa kamati hiyo kukagua miradi ya kimkakati inayoendelea kutelelezwa katika Manispaa hiyo.
Wajumbe hao wametembelea na kukagua ujenzi wa soko la Mwanga unaoendelea ukiwa umefikia 68% ya ujenzi, ujenzi wa soko la samaki katika mwalo wa Katonga ukiwa umefikia 39% na ujenzi wa soko la samaki katika Mwalo wa Kibirizi ukiwa hatua ya kujaza kifusi.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Gregory Keberezo amewataka Wataalamu kuendelea kusimamia kikamilifu ujenzi wa miradi hiyo ya uwekezaji na inayoboresha miundombinu na Mazingira rafiki kwa Wafanyabishara na kukuza Mapato ya Halmashauri.
