Joy FM

Kanisa lanunua magari kuimarisha uchumi wa kanisa Kasulu

12 May 2026, 09:48

Askofu Emmanuel Bwatta katika picha ya pamoja na katibu tawala wa wilaya ya Kasulu Bi. Theresia Mtelewe, Picha na Hagai Ruyagila

Makanisa yana umuhimu mkubwa wa kuanzisha miradi ya kuongeza kipato kwa sababu yanasaidia kuimarisha huduma za kiroho na maendeleo ya jamii kwa ujumla

Na Hagai Ruyagila

Katika jitihada za kusaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira hapa nchini, Dayosisi ya Western Tanganyika Kanisa Anglikana Tanzania limenunua magari mawili aina ya Tata kwa ajili ya shughuli za usafirishaji wa abiria jambo ambalo kitasaidia baadhi ya vijana kupata ajira.

Katibu tawala Bi. Theresia Mtelewe akizungumza katika hafla ya kupokea magari aina ya tata makao makuu ya ofisi ya kanisa Anglika Tanzania Dayosisi ya Western Tanganyika, Picha na Hagai Ruyagila

Akizungumza katika hafla ya kupokea magari hayo, Askofu Emmanuel Bwatta wa Dayosisi hiyo, amesema kuwa ununuzi wa magari hayo ni sehemu ya mikakati ya Dayosisi katika kuinua uchumi wa kanisa pamoja na kutoa fursa za ajira kwa vijana na wananchi wa eneo hilo.

Amesema kuwa magari hayo yatasaidia kuongeza mapato ya Dayosisi huku yakitoa huduma ya usafiri kwa wananchi, jambo ambalo litachochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika wilaya ya Kasulu na maeneo ya jirani.

Sauti ya Askofu Emmanuel Bwatta
Katibu tawala akikata utepe wakati wa uzinduzi wa magari mawili yaliyonunuliwa na Kanisa, Picha na Hagai Ruyagila

Katibu Tawala wa Wilaya ya Kasulu Bi. Theresia Mtelewe, amepongeza Kanisa hilo kwa hatua hiyo akieleza kuwa uwekezaji huo utaongeza ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi wa kanisa pamoja na taifa kwa ujumla kwani kanisa linakwenda kujitegemea.

Sauti ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Kasulu Bi. Theresia Mtelewe

Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika, Ohadi Mdunya amesema ni vizuri kuwa na maoni yenye matokeo kama ambavyo askofu Bwatta anavyofanya ili kufanikisha miradi mingine ya maendeleo yenye lengo la kuimarisha uchumi wa kanisa.

Sauti ya Ohadi Mdunya
Muonekano wa magari yaliyonunuliwa na Kanisa kama sehemu ya mradi wa kanisa, Picha na Hagai Ruyagila

Naye mwenyekiti wa maendeleo Kanisa kuu la Mt. Andrea Anglikana Kasulu Mjini Zabron Nashon amesema kuwa wana Fanya hivyo ili kutotegemea sadaka pekee bali kuanzisha miradi ambayo itasaidia Dayosisi hiyo kusonga mbele kiuchumi.

Sauti na Zabron Nashon