Joy FM

DC Kasulu: NGOs zijijenge kifedha kuwa na uendelevu wa miradi

24 July 2026, 09:51

Picha ya pamoja baada ya kikao Cha mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na Katibu tawala wa wilaya ya Kasulu Bi, Theresia Mtelewe baada ya kukaimu nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu, Picha na Hagai Ruyagila

Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yana mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii kupitia utoaji wa huduma za afya, elimu, mazingira, kilimo, haki za binadamu na sekta nyingine nyingi hata hivyo, mashirika mengi yamekuwa yakitegemea fedha kutoka kwa wafadhili wa nje, hali ambayo wakati mwingine huathiri utekelezaji wa shughuli zake

Na Hagai Ruyagila

Mkuu wa wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma, Kanali Isaac Mwakisu, ameyataka mashirika yote yasiyo ya kiserikali (NGOs) Wilayani humo kujenga vyanzo mbalimbali vya upatikanaji wa fedha ili kuhakikisha shughuli zao zinaendelea kwa ufanisi hata pale mfadhili mmoja anapositisha au kuondoka katika ufadhili.

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu, Picha na Hagai Ruyagila

Kanali Mwakisu ametoa wito huo wakati akifungua kikao cha robo ya mwaka kuanzia April hadi Juni 2026 cha Jukwaa la mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) wilayani Kasulu

Amesema utegemezi wa mfadhili mmoja unaweza kuhatarisha utekelezaji miradi na utoaji wa huduma kwa wanancha, hivyo ni muhimu kwa mashirika hayo kupanua wigo wa ushirikiano kwa kujenga mitandao na wadau mbalimbali wa maendeleo ili kuimarisha uendelevu wa shughuli na program wanazotekeleza katika jamii.

Sauti ya Kanali Isaac Mwakisu

Kaimu Msajili msaidizi wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali halmashauri ya Mji Kasulu Godfrey Jeremiah amesema yapo Mashirika yamekuwa yakishindwa kujiendesha yenyewe kutokana na kutegemea wafadhili ndiyo maana hata mfadhili mwenyewe anapenda kuweka fedha zake sehemu ambayo shirika linaweza kujiendesha lenyewe.

Sauti ya Godfrey Jeremiah
Kaimu msajili msaidizi wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali halmashauri ya Mji Kasulu, Godfrey Jeremiah, Picha na Hagai Ruyagila

Washirki waliohurulia kikao hicho wameunga mkono hoja ya mkuu wa wilaya ya Kasulu kuhakikisha kila anayeanzisha NGOs anakuwa na uwezo ya kuiendesha kuliko kutegemea zaidi wafadhili jambo ambalo limepelekea baadhi ya NGOs kushindwa kujiendesha zenyewe.

Sauti ya wadau wa Mashirika