Joy FM
Joy FM
27 April 2026, 14:41

Wananchi katika Halmashauriya Mji wa Kasulu Mkoani Kigoma wametakiwa kuendelea kuchukua hatua za kudhibiti ugonjwa Malaria kwa kuweka salama mazingira na kufukia madibwa katika maeneo yao
Na Emmanuel Kamangu
Imeelezwa watu saba hadi kumi katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu Mkoani Kigoma hufariki kila mwaka kutokana na ugongwa wa Malaria.
Amebainisha hayo mratibu wa kudhibiti ugonjwa malaria katika Halmashauri ya mji wa kasulu Bw. Giribeti Moshi katika maadhimisho ya siku ya malaria Dunia maadhimisho ambayo yamefanyika kwa kusafisha maeneo mbali mbali ya mji wa kasulu ikiwemo kufukia madimbwi ambayo ni rafiki na mazalia ya mbu.

Aidha Bw, Moshi amewasihi sana wanajamii wakiwemo wanafunzi ambao wameshiriki maadhimisho haya kuachana na tabia kutumia dawa pasipo kupima ikiwemo kuacha tabia ya kutokumaliza dozi wanapobainika kuwa na ugonjwa wa malaria.
Naye afisa afya Halmashauri ya mji wa kasulu Bw, malimi ntemiseni amesema kuna kila sababu ya jamii nzima kwa ujumla kuhakikisha inatambua umhimu wa kusafisha mazingra wanayoishi ili kukabiliana na magonjwa mbali mbali ikiwemo ugonjwa wa malaria.
Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi pamoja na wanachi wakitoa maoni yao baada ya kuhitimisha zoezi la usafi wamesema wanawajibu wa kuendelea kuhakikisha wanafyeka vichaka na kufukia madimbwi ili kuondokana na ugonjwa hatari wa malaria.

Siku ya malaria Duniani huadhimishwa tarehe 25 April ya kila mwaka ikiwa ni mkakati wa serikali katika kuendelea kuongeza uelewa kwa wananchi juu ya njia za kupambana na ugonjwa wa malaria.