Joy FM
Joy FM
10 June 2026, 14:54

Katibu tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amewataka wananchi wa Mkoa wa Kigoma kutoa ushirikiano na kulinda miradi ya maendeleo ambao inaendelea kutekelezwa
Na Mwandishi wetu
Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Kampasi ya Kigoma, umefikia Asilimia 78.9 huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Agosti,2026.

Kukamilika kwa ujenzi wa taasisi hiyo kunatoa fursa ya udahili wa kwanza kwa wanachuo watakaohitaji kusoma katika kampasi hiyo mwaka wa masomo 2026, jambo litakaloongeza fursa za kitaaluma kwa kada ya Afya na kuimarisha Sekta ya matibabu mkoani Kigoma na maeneo jirani.
Akizungumza mara baada ya kukagua Maendeleo ya ujenzi wa mradi huo, Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma CPSP. Hassan Rugwa amesema kwa sasa Serikali inaendelea kukamilisha miundombinu muhimu ikiwemo barabara ili kulifanya eneo hilo kufikika kwa urahisi.

Amesema Taasisi hiyo ni kiungo muhimu hivyo wakazi wanapaswa kuchangamkia fursa mbalimbali zitakazojitokeza kutokana na uwepo wa chuo hicho.
Naye Mhandisi Mkazi wa mradi huo Selemani Malambo, amesema kazi zote za msingi katika ujenzi huo zimekamilika huku zikibaki kazi chache za ukamilishaji wa miundombinu ya ndani sambamba na usawazishaji wa ardhi nje ya majengo hayo.
