Joy FM

Zaidi ya wananchi 2500 kunufaika na kambi ya madaktari bingwa Kigoma

1 June 2026, 14:35

Katibu tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa akiwa katika uzinduzi wa madaktari bingwa, Picha na TimotheoLeonard

Kambi ya madaktari ni mpango wa muda mfupi unaowaleta wataalamu wa afya katika jamii ili kutoa huduma za matibabu, uchunguzi na elimu ya afya na kambi hizi zina umuhimu mkubwa katika kuboresha afya ya wananchi, hasa katika maeneo ya vijijini ambako huduma za afya ni chache

Na Timotheo Leonard

 Zaidi ya wananchi elfu mbili na mia tano Mkoani Kigoma, wanatarajia kunufaika na kambi ya siku tano ya madaktari bingwa na ubingwa bobezi inayolenga kusogeza huduma za kibingwa karibu na jamii.

Kambi hiyo imezinduliwa rasmi leo Juni Mosi, 2026 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma Maweni, na Katibu Tawala wa Mkoa Hassan Rugwa, ambapo itahitimishwa tarehe tano Juni 2026.

Katibu tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa mwenye Suti akiwa katika uzinduzi wa madaktari bingwa, Picha na Timotheo Leonard

Rugwa amebainisha kuwa uwepo wa kambi hiyo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza usumbufu na gharama kwa wananchi, ambao walilazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hizo mikoa mingine ikiwemo Dodoma na Dar es Salaam.

Sauti ya Katibu Tawala wa Mkoa Hassan Rugwa

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Maweni, Daktari Joseph Nangawe, amewataka wananchi kuchamkia fursa hiyo adhimu, huku akifafanua kuwa kambi hizo zimekuwa zikiendeshwa kila robo mwaka na zimeleta matokeo chanya.

Sauti ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Maweni, Daktari Joseph Nangawe

Nao baadhi ya wananchi waliojitokeza kupata matibabu hayo, wameishukuru serikali kwa kusogeza huduma hizo mlangoni mwao, wakisema hatua hiyo imewaokoa na safari ndefu za kutafuta matibabu.

Sauti ya wananchi Kigoma

Kambi ya madaktari ni mpango wa muda mfupi unaowaleta wataalamu wa afya katika jamii ili kutoa huduma za matibabu, uchunguzi na elimu ya afya na kambi hizi zina umuhimu mkubwa katika kuboresha afya ya wananchi, hasa katika maeneo ya vijijini ambako huduma za afya ni chache.