Joy FM

Serikali kuendelea kuboresha ustawi wa wazee Kigoma

14 July 2026, 15:25

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhandisi Maryprisca Mahundi, akizungumza na baadhi ya wadau Picha na Lucas Hoha

Wazee ni hazina ya taifa na msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na wametumia nguvu, maarifa na uzoefu wao katika kujenga taifa na kulea vizazi mbalimbali kutokana na mchango wao mkubwa, serikali ina wajibu wa kuhakikisha wanapata huduma na ulinzi unaostahili ili waishi maisha yenye heshima na ustawi

Na Lucas Hoha

Serikali imeahidi kuendelea kuboresha mazingira ya maisha ya wazee wasiojiweza nchini kupitia utoaji wa bima ya afya na uboreshaji wa miundombinu ya makazi yao ikiwa ni sehemu ya kuthamini mchango wa wazee kwenye jamii.

Akizungumza baada ya kutembelea Kituo cha Makazi ya Wazee Wasiojiweza cha Silabu kilichopo Kata ya Kibirizi, Manispaa ya Kigoma Ujiji, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema wazee wanapaswa kuthaminiwa na kuheshimiwa kwa kuwa wameendelea kuwa nguzo muhimu katika jamii.

Sauti ya Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhandisi Maryprisca Mahundi

Awali, Afisa Ustawi wa Jamii na Msimamizi wa Makazi ya Wazee wasiojiweza Silabu, Binura Abbas Joshua, amesema kituo hicho kinaendelea kuwahudumia wazee kwa ushirikiano kati ya serikali na wadau wa maendeleo, wakiwemo shirika la Joy in The Harvest, ambao wamekuwa wakichangia huduma mbalimbali kwa ustawi wa wazee hao.

Sauti ya Afisa Ustawi wa Jamii na Msimamizi wa Makazi ya Wazee wasiojiweza Silabu, Binura Abbas Joshua

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua, ameipongeza Serikali kwa juhudi zinazoendelea kufanyika katika kuwahudumia wazee wasiojiweza, ikiwemo kuwawezesha kupata huduma za afya, chakula na mavazi.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya Kigoma
Baadhi ya wazee wa SILABU wakiwakatika picha na wananchi walijitokeza kwenye hafla hiyo, Picha na Lucas Hoha

Kituo cha kulea na kutunza wazee wasiojiweza cha SILABU Kilichopo Manispaa ya Kigoma Ujiji kina jumla ya wazee 22 wanawake wakiwa 10 na wanaume wakiwa ni 12