Joy FM
Joy FM
16 April 2026, 9:38 am

Fursa nyingi za kiuchumi ambazo bado hazijatumika kikamilifu na kuleta tija ya kiuchumi kwa wananachi na taifa kwa ujumla zimeelzwa kuwepo katika Mkoa wa Kigoma
Na Lucas Hoha
Naibu waziri wa Viwanda na Biashara nchini Tanzania David Londo amewahakikisha wawekezaji kutoka jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa serikali imeufungua Mkoa wa Kigoma kuwa wa Kibiashara na kuwataka wawekezaji kujitokeza kuwekeza ili kukuza uchumi kwa maendeleo ya nchi za Afrika Mashariki.
Naibu waziri wa biashara Mh. Londo ameyasema hayo wakati akifungua Kongamano la Biashara na uwekezaji la Ziwa Tanganyika ambalo limefanyika mjini Kigoma
Amesema uwepo wa Ziwa Tanganyika ambalo linaunganisha nchi zaidi ya tatu 3 ikiwemo Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni mlango muhimu utakaowezesha biashara kufanyika kwa ufanisi.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro ametaja baadhi ya miradi ya kimkakati ambayo imetekelezwa na serikali katika ikiwemo kupatikana na umeme wa uhakika, ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami na uboreshaji wa Meli ya Mv. Liemba ambao umefikia zaidi ya asilimia 50.
Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara wa Mkoa wa Kigoma wamesema serikali kuufungua mkoa wa kigoma ni suala muhimu, huku wakiomba kuwepo kwa ushirikiano baina ya nchi zinazozunguka ziwa Tanganyika ili kuboresha usafiri na usafirishaji wa bidhaa na abiria katika Ziwa hilo.
Kongamano hili linaonesha taswira madhubuti ya jitihada za serikali za kuifanya Kigoma kama eneo la kimkakati kw kuwa kitovu cha biashara kwa biashara za mpakani kwa nchi zinazozunguka Ziwa Tanganyika kama Burundi, Rwanda, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo