Joy FM

Mashirika yasiyo ya kiserikali yatakiwa kuwa na umoja

7 July 2025, 09:39

Wanajukwaa kutoka mashirika mbali mbali yaliyopo Wilayani Kasulu wakiwa katika mkutano wa mashirika yasiyo ya kiserikali, Picha na Emmanuel Kamangu

Mkuu wa Wilaya Kasulu Mkoani Kigoma Kanali Isac Mwakisu amesema anatamani kuona mashirika yasiyo ya kiserikali yakishikamana na kufanya kazi kwa umoja katika kuwahudumia wananchi kupitia shughuli mbalimbali za kijamii

Na Emmanuel Kamangu

Mashirika zaidi ya 40 yasiyo ya kiserikal Wilayani Kasulu yametakiwa kufanya kazi kwa ushirika ili kujikwamua kiuchumi na kufanya kwa urahsi shuguli za kijamii.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kasulu kanal Isack  Mwakisu akiwa katika jukwa  la mashirika yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi zake wilayani humo  ambapo amewasihi kufanya kazi kwa umoja  ili kuharakisha maendeleo katika jamii.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu kanal Isack  Mwakisu
Mkuu wa Wilaya Kasulu Kanali Isac Mwakisu akihutubia washiriki wa jukwaa la mashirika yasiyo ya kiserikali.

Aidha Kanal Mwakisu ameyapongeza mashirika hayo kwa jinsi yanavyofanya kazi nzuri za kijamii huku akiahidi kuendelea kutoa ushirikiano ili kuhakikisha yanasimama imara.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu kanal Isack  Mwakisu

Baadhi ya wa wakikilishi kutoka mashirika mbali mbali ambayo  yameshiriki jukwa hili la mashirika yasiyo ya kiserikali Wilayani Kasulu wameiomba serikali kuendelea kuwashika mkono katika kuhakikisha wanapata fursa ya kujikwamua kiuchumi.

Sauti ya baadhi ya wa wakikilishi kutoka mashirika mbali mbali ambayo  yameshiriki jukwa hili la mashirika yasiyo ya kiserikali

Mashirika hayo ambayo hufanya shuguli zake wilayani kasulu yameazimia kufanya kazi kwa umoja  ikwa ni pamoja na kushirikishana changamoto zinazowakabili hasa kwa kipindi hiki ambacho mashirika mengi yanakabiliwa na ukata mkubwa ili kufanya vema shuguli za kijamii.