Joy FM

Zaidi ya vibanda 50 soko la kijiji cha Mvinza vyateketea kwa moto Kasulu

23 June 2026, 11:38

Muonekano wa maduka yaliyoteketezwa na moto Kijiji cha Mvinza Kasulu, Picha na Mwandishi wetu

Moto ni janga linaloweza kusababisha hasara kubwa kwa muda mfupi sana linavyoweza kuathiri maisha ya watu na uchumi wa jamii kwa ujumla

Na Mwandishi wetu

Zaidi ya vibanda 50 vya wafanyabiashara katika soko la kijiji cha Mvinza kata ya Kagerankanda Halmshauri ya Wilaya ya Kasulu Mkoani kigoma vimeteketea moto kutokana na hitilafu ya Umeme na kusababisha hasara kwa Wafanyabiashara katika Soko hilo.

Akizungumza kwa njia ya Simu Mwenyekiti wa kijiji cha Mvinza Denis Kavula Amesema moto huo ulizuka majira ya saa tano usiku wa kuamkia leo june 23 ambapo jitihada za kuzima moto huo zilishindikana licha ya wananchi kufanikiwa kuokoa baadhi ya mali za wafanya biashara hao.

Muonekano wa maduka yaliyoteketezwa na moto Kijiji cha Mvinza Kasulu, Picha na Mwandishi wetu

Amesema chanzo cha Moto huo unadhaniwa kuwa ni hitilafu ya umeme iliyotokea katika vibanda viwili vya soko hilo huku akieleza kuwa athari imekuwa kubwa kutokana na bidhaa za wananchi kuteketea kwa moto.

Saut ya Mwenyekiti wa kijiji
Muonekano wa vibanda viliyoteketezwa na moto Picha na Mwandishi wetu

Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Mvinza kata ya Kagerankanda wameliomba Jeshi la zima moto na Uokoji Wilaya ya Kasulu kuendelea kutoa elimu ya namna ya kukabiliana na majanga ya Moto ili kuendelea kuchukua tahadhari pindi majanga hayo yanapotokea