Joy FM
Joy FM
20 April 2026, 13:57

Wazazi na walezi wametakiwa kuona umuhimu wa ushirikiano kati ya wadau wa elimu katika kutatua changamoto zinazoikabili shule ya Sekondari Kigoma Grand
Na Hagai Ruyagila
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kasulu, mkoani Kigoma Mwalimu Vumilia Simbeye ameahidi kuchangia tofali 5000 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa uzio katika shule ya sekondari Kigoma Grand, Hatu hiyo ni sehemu ya juhudi za kuboresha mazingira ya kujifunzia pamoja na kuimarisha usalama wa wanafunzi na mali za shule.
Mwl. Simbeye ametoa ahadi hiyo wakati akijibu changamoto mbalimbali zilizowasilishwa kupitia risala ya shule, katika mahafali ya wanafunzi wa kidato cha sita yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano Samia hall shuleni hao.

Aidha amewahimiza wazazi na walezi kushirikiana na uongozi wa shule kwa kuchangia maendeleo yake, hususan katika kukamilisha ujenzi wa uzio huo.
Awali akisoma risala katika mahafali hayo Mkuu wa shule ya sekondari Kigoma Grand, Mwalimu Severino Manyota, amezungumzia changamoto ya uzio na baadhi ya mafanikio.

Mwenyekiti wa Bodi wa shule hiyo Henry Mpabandi amemshukuru mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kasulu kwa namna alivyoahidi kuchangia tofali hizo na kuhamasisha wazazi kuchangia shughuli za maendeleo.