Joy FM

Kina baba watakiwa kushiriki kliniki za baba, mama na mtoto Kasulu

13 June 2026, 15:21

Mkunga wa kituo Cha afya kiganamo Bi Sarafina, Picha na Emmanuel Kamangu

Serikali imewaasa kina mama kuambatana na wenza wao wanapoenda kliniki ikiwa ni mojawapo ya mkakati wa kujabiliana na vifo vya watoto

Na Emmanuel Kamangu

Wenza katika Halmashauri ya mji wa kasulu wametakiwa kushiriki kikamilifu kiliniki  ya baba na mama  ili kukabiliana na vifo vya mama na mtoto vinavyoweza kujitokeza baada na  kabula ya kujifungua.

Wito huo umetolewa na Bi. Sarafina  Chonko  ambaye ni mkunga  kutoka  kituo cha afya kiganamo halmashauri ya mji wa kasulu  kwa niaba ya mratibu wa kukabiliana na vifo vya mama na mtoto ambapo amesema kuna kila sababu wenza kuwasindikiza wajawazito kiliniki ili kupewa njia bora ya kuendelea kumtunza kiafya mama mjazito .

Aidha Bi. Kachonko amebainisha kuwa wanaendelea kuchukua hatua mbali mbali za kiafya kwa mama mjamzito ili kuhakikisha anakuwa salama kabla na baada ya kujifungua ikiwa ni kukabiliana na vifo vya mama mtoto

Bi Sarafina chonko akiwa amemaliza kutoa huduma ya uzazi kwa mama mjamzito katika kituo Cha afya kiganamo, Picha na Emmanuel kamangu.

Hata hivyo Bi Kachonko amesema wenza wanatakiwa kutambua dalili za hatari kwa mama mjamzito na baada ya kujifungua kwani hii itasaidia kuendelea kuimalisha  usalama wa mama na mtoto alieko tumboni.

Kituo cha afya kiganamo hutuoa  huduma kwa wajawazito zaidi ya miatatu  kila mwezi ikitajwa ongezeko hili ni kutokana na elimu ya afya ya uzazi inayoendelea kutolea  na watalamu wa  afya kwa wananchi.

Sauti ya Mwandishi wetu Emmanuel Kamangu