Joy FM
Joy FM
24 June 2026, 17:51

Walimu walipokea madawati hayo wametakiwa kutatunza ili yaweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu
Na Mwandishi wetu
Benki ya NMB imekabidhi madawati 150 kwa shule mbalimbali za Wilaya ya Kakonko katika hafla iliyofanyika leo, Juni 24, katika Shule ya Msingi Kiyobela.
Hafla hiyo imehudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko, Mustapha Mtungwe, Afisa Elimu ya Awali na Msingi, Isabella Mwakabonga, Mdhibiti Ubora wa Shule Wilaya, Japhet Mbaga pamoja na Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Kakonko Bi.Elizabeth Kanjagaile.



Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Elimu ya Awali na Msingi, Isabella Mwakabonga ameishukuru Benki ya NMB kwa mchango huo mkubwa ambao unaenda kusaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia kwa wanafunzi wa wilaya hiyo.
Amesema madawati hayo yatasaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa samani za shule na kuongeza ari ya wanafunzi katika masomo.

Kwa upande wake, Meneja wa NMB Kakonko, amesema benki hiyo itaendelea kushirikiana na jamii katika kusaidia sekta ya elimu kadri itakavyowezekana.
Naye Mdhibiti Ubora wa Elimu Wilaya ameishukuru NMB kwa moyo wake wa kujitolea na kuahidi kufuatilia matumizi sahihi ya madawati hayo ili yafikie lengo lililokusudiwa.
Akihitimisha hafla hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Mustapha Mtungwe aliwataka walimu, wanafunzi na kamati za shule kuyatunza madawati hayo kwa umakini ili yadumu kwa muda mrefu na kuendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia.
Amesisitiza kuwa utunzaji bora wa miundombinu ya elimu ni msingi muhimu wa kuinua ufaulu na maendeleo ya wanafunzi.