Joy FM

Kasulu yavuka lengo la ukusnyaji mapato

5 May 2025, 15:17

Madiwani wakiwa katika baraza la madiwani Halmashauri ya Mji wa Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila

Halmashauri ya Mji wa Kasulu Mkoani Kigoma imevuka lengo la ukasanyaji wa mapato ya ndani kwa asilimia 102.

Na Hagai Ruyagila

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji Kasulu mkoani Kigoma limempongeza Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Mwl, Vumilia Simbeye kwa kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa asilimia 102 sawa na zaidi ya Bilioni 2 na milioni 263 ya makisio na makadilio kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Kasulu Mh, Selemani Kwirusha ametoa pongezi hizo katika mkutano wa baraza la madiwani katika robo ya tatu kipindi cha Januari mpaka Machi kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Kasulu Mh, Selemani Kwirusha, Picha na Hagai Ruyagila

Halmashauri hiyo mpaka sasa imekusanya zaidi ya shilingi bilioni 2 na milioni 263 sawa na asilimia 102 ambapo mapato hayo yatasaidia katika shughuli za maendeleo kwa sekta ya elimu, afya na miundombinu ya barabara.

Sauti ya Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Kasulu Mh, Selemani Kwirusha

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Mwl, Vumilia Simbeye amesema mapato hayo yameongezeka kwasababu ya umakini wa ukusanyaji wao wa mapato.

Sauti ya Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Mwl, Vumilia Simbeye

Baadhi ya madiwani wanaeleza siri ya wao kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato hayo kabla hata ya mwaka kutamatika hatua ambayo imekuwa changamoto katika halmashauri nyingine wao wamewezaje.

Sauti ya Baadhi ya madiwani wanaeleza siri ya wao kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato

Na hapa Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kasulu Mwl, Vumilia Simbeye anatoa wito kwa wafanyabiashara na wananchi wa Mjini Kasulu kuona namna ambavyo suala la kodi haliepukiki maana shughuli za miradi ya maendeleo zinatokana na kodi wanazozitoa.

Sauti ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kasulu Mwl, Vumilia Simbeye