Joy FM
Joy FM
22 April 2026, 15:46

Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji imeanza kutekeleza zoezi la uondaaji wa taka zilipo katika vizimba ikiwa ni mkakati wa kufanya mji wa Kigoma kuwa msafi
Na Mwandishi wetu
Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kigoma Mjini imeilekeza idara ya mazingira ya Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, kuboresha hali ya usafi kwa kuondoa taka ambazo zimekuwa zikizagaa ovyo katika baadhi ya maeneo.
Hatua hiyo ni baada ya wajumbe wa kikao cha Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Kigoma kueleza kuwa hali ya usafi wa mazingira katika maeneo mbali mbali ya Manispaa ya Kigoma Ujiji hairidhishi ikiwemo maeneo yaliyowekwa vizimba kwa ajili yaa kukusanyia uchafu.

Awali akijibu hoja za wajumbe wa kikao hicho Afisa Mazingira Manispaa ya Kigoma Ujiji, ameelezza baadhi ya mikakati iliyopo ya kuondoa taka zinazozagaa ili kuweka mazingira ya mji katika hali ya usafi.
Katibu wa CCM Wilaya ya Kigoma Mjini Sadick Kadulo aliyeongoza kikao hicho kwa niaba ya Mwenyekiti Ahmed Mwilima, ameitka idara hyo kuongeza bidii ya usafi wa mazingira hasa katika maeneo yaliyokithiri kwa uchafu.