Joy FM
Joy FM
7 May 2026, 12:34

Kikao hicho kinalenga kujadili namna bora ya kuendelea kushirikisha jamii katika masuala ya usalama na kuimarisha dhana ya polisi jamii katika maeneo yao
Na Mwandishi wetu
Kamishna wa Polisi Jamii CP Alex Mkama leo Mei 7,2026 amewasili Mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi ambapo amepokea taarifa ya hali ya usalama na kuwataka askari kuendelea kuimarisha usalama wa raia na mali zao.
Akiwa Mkoani Kigoma atafanya kikao kazi na viongozi wa Serikali za mitaa/Vijiji, Kata na viongozi wa dini na Polisi kata kwa lengo la kuhamasisha jamii kuendelea kutii sheria bila shuruti na kushiriki kubaini, kuzuia na kutanzua uhalifu.

Sambamba na hilo, CP Mkama amehimiza wananchi kuendelea kutii sheria bila kushurutishwa na kushiriki kikamilifu katika kubaini, kuzuia na kutanzua uhalifu.
Amesema usalama wa nchi ni jukumu la kila mwananchi, hivyo ni muhimu jamii kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa sahihi na kwa wakati ili kudhibiti vitendo vya uhalifu kabla havijatokea au kuleta madhara kwa jamii.
