Joy FM
Joy FM
8 August 2024, 09:56

Mkuu wa wilaya buhigwe Michael Ngayalina amelitaka jeshila Polisi wilayano humo kuwachukulia hatua za kisheriamadereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani ili kupunguza ajali.
Na Michael Mpunije – Buhigwe
Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani wilayani Buhigwe Mkoani Kigoma Limetakiwa kusimamia sheria za usalama barabarani kwa kuwatoza faini waendesha vyombo vya moto kulingana na kosa wanapobainika kukiuka sheria za usalama Barabarani.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Buhigwe kanali Michael Ngayalina wakati akijibu malalamiko ya wananchi wa kijiji cha Songambele wilayani humo.
Kanali Ngayalina amesema watashughulikia malalamiko ya wananachi na kuhakikisha sheria za usalama barabarani zinazingatiwa ili kupunguza ajari za barabarani zinazotokana na uzembe wa madereva.
Aidha ameongeza kwa kuwataka waendesha vyombo vya moto wilayani Buhigwe kufuata sheria za Usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kuheshimu vizuizi vinavyowekwa katika maeneo ambayo ujenzi wa barabara unaendelea.
Kwa upande wao baadhi ya waendesha pikipiki maarufu Bodaboda wilayani Buhigwe wameliomba jeshi la polisi kuendelea kufuatilia baadhi ya madereva wanaokiuka sheria ili waweze kuchukuliwa hatua kwa lengo la kupungunza ajari barabarani.