Joy FM

Msichana miaka 15 adaiwa kubakwa na mjomba wake Kigoma

17 January 2024, 10:22

Binti  mmoja  mwenye umri wa miaka 15 ambaye ni mhitimu wa elimu ya msingi mwaka jana amekutana na madhira ya kubakwa na mjomba wake ambaye ni mdogo wa mama yake alipokwenda kumsalimia.

Na, Josephine Kiravu

Ni binti Zulekha Hussein sio jina lake halisi akieleza hali ilivyokuwa kabla ya mjomba wake huyo kufanya tukio hilo la kumbaka.

Na hapa anasimulia namna tukio hilo lilivyokuwa.

Binti huyu anaendelea kusema kuwa baada ya tukio hilo mjomba wake alijaribu kumshawishi akaye kimya huku akiahidi kumpatia fedha ama nyumba yake anayoishi.

Kwa mujibu wa Zulekha amelelewa na shangazi yake baada ya wazazi wake kutengana na ameishi hapo hadi alipohitimu elimu ya msingi mwaka jana lakini ilikuaje binti huyo akaenda kuishi kwa bibi yake?

shangazi

Sikuishia hapa imenilazimu kumtafuta Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma ACP Filemon Makungu ili kufahamu endapo wanalitambua tukio hili na hatua zilizochukuliwa.

RPC Makungu

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi Mkoa wa Kigoma ACP Filemon Makungu katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Disemba 2023 washtakiwa wa 9 wa makosa ya ubakaji katika mahakama ya wilaya ya Uvinza, Kigoma, kasulu, Kibondo, Kakonko na Buhigwe wamehukumiwa kifungo cha kwenda jela kwa miaka 30,  huku mshtakiwa mmoja katika wilaya ya kasulu akiwa amehukumiwa kifungo cha kwenda jela miaka 45 na washtakiwa wengine 2 katika mahakama ya wilaya ya kibondo na Kigoma wamehukumiwa kifungo cha kwenda jela maisha kwa kosa la kulawiti.