Joy FM
Joy FM
22 April 2026, 14:57

Kujiepusha na mikopo ya kausha damu kunasaidia kulinda uhuru wa kifedha, afya ya akili, na heshima ya mtu binafsi.
Na Michael Mpunije
Wenyeviti wa Serikali za mitaa katika Kata ya Nyansha halmashauri ya Mji Kasulu Mkoani Kigoma wametakiwa kutoa elimu kwa wananchi wao kujiepusha na mikopo umiza maarufu kausha damu ambayo imekuwa ikiathiri malengo yao na kuwarudisha nyuma Kiuchumi hasa wanaposhindwa kulipa madeni.