Joy FM

DC Chuachua aagiza watendaji kupiga faini wanaochafua mazingira

19 September 2026, 10:45

Mkuu wa Wilaya Kigoma Dkt. Rashid Chuachua akiwa kwenye guta wakati akigawa kwa viongozi ili kusaidia katika usafi wa mazingira, Picha na Lucas Hoha

Usafi wa mazingira ni jambo muhimu katika maisha ya binadamu na mazingira safi humsaidia mtu kuishi katika hali nzuri na humkinga dhidi ya magonjwa mbalimbali

Na Lucas Hoha

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashird Chuachua amewaagiza Watendaji wa kata zilizopo Manispaa ya Kigoma Ujij kuwatoza faini wananchi wanaochafua Mazingira kwa kutupa taka ovyo ili kuhakikisha Manispaa ya Kigoma Ujiji na maeneo mengine ya Wilaya hiyo yanakuwa safi muda wote.

Mkuu wa Wilaya Kigoma akikabidhi funguo ya guta kwa afisa mtendaji kwa ajili kutumika katika shughuli za usafi wa mazingira, Picha na Lucas Hoha

Chuachua  ameyasema hayo wakati akikabidhi Pikipiki za miguu Mitatu maarufu kama Guta kwenye idara ya usafi wa Mazingira Katika Manispaa ya Kigoma Ujiji ambazo zinatafanya usafi kwa baadhi ya Kata za Manispaa hiyo ikiwemo Kata ya Mwanga Kaskazini na Kata ya Gungu

Amesema ili kukomesha tatizo la baadhi ya watu wanaochafua mazingira kwa makusudi sasa watendaji wa kata wataanza kukamata watu wa wanaochafua mazingira nakuwatoza faini pale inapobidi

Baadhi ya maguta yaliyotolewa kwa ajili ya kutumika katika shughuli za usafi wa mazingira, Picha na Lucas Hoha

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Mussa Maulid pamoja n mambo mengine amewataka watendaji wa kata ambao wamepewa Maguta hayo kuhakikisha wanayatunza ili yafanye kazi ya usafi kwa muda mrefu

Awali Afisa Usafi wa Mazingira katika Manispaa ya Kigoma Ujiji Petronila Gwakila akitoa taarifa ya pikipiki za Miguu Mitatu amesema zimeghalimu zaidi ya shilingi Milioni 50 ambazo zimetengwa kutokana  na mapato ya ndani lengo likiwa ni kurahisisha shughuli za usafi wa mazingira katika Manispaa hiyo

Mkuu wa Wilaya Kigoma akikabidhi funguo za bima kwa viongozi wa serikali za mitaa, Picha na Lucas Hoha