Joy FM
Joy FM
2 September 2026, 13:42

Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini mkoani Kigoma ameanzisha mashindano ya mpira wa miguu yenye lengo la mashindano hayo ni kukuza vipaji na kudumisha mshikamano miongoni mwa jamii.
Na Sadick Kibwana
Ligi ya mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Mhe. Kiza Mayeye (Mayeye Cup), imeanza rasmi Jumanne hii, Septemba 1, 2026, katika uwanja wa tarafa ya Mwandiga ikihusisha jumla ya timu 32.

Akizungumza kwa niaba ya Mbunge huyo, Katibu wa Mbunge, amesema lengo la ligi hiyo ni kuwapa fursa vijana kwa kukuza vipaji, kuonekana, na kujipatia kipato.
Aidha, Mwenyekiti wa Mashindano hayo, Bw. Dotto Kondo, amesema ligi hiyo inaanza kwa kuhusisha timu zilizo ndani ya jimbo hilo pekee lenye kata 16.
Naye Katibu wa chama cha soko Wiliya Kigoma DOKFA, Dumango Yahaya amepongeza mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini Kiza Mayeye kwa kuanzisha mashindano hayo ambayo yatasaidia kuibua vipaji kwa vijana mbali na kuleta mshikamano kwa wananchi wa jimbo hilo.
Ligi ya Mayeye Cup 2026 inafanyika kwa mara ya kwanza tangu mbunge huyo apate nafasi ya kuongoza Jimbo la Kigoma Kaskazini, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi alizozitoa kwa vijana wa jimbo hilo.
