Mazingira FM
Mazingira FM
19 August 2026, 10:20 am

Wanaiomba serikali iweze kuingilia kati suala hili ili waweze kupata maji safi na salama kwa wakati muafaka
Na Juma Hangi
Wakazi wa Bunda Mjini wamelalamikia kukatika kwa huduma ya maji kwa siku nne hadi wiki nzima, wakisema hali hiyo inakwamisha shughuli za uzalishaji Pamoja na matumizi ya kawaida ya nyumbani.
Wakizungumza leo, Agosti 18, 2026, wakazi hao wameiomba serikali na mamlaka husika kuchukua hatua za haraka kukabiliana na changamoto hiyo, wakisisitiza kuwa maji ni uhai na bila maji shughuli nyingine za kila siku zinakwama.
wanaiomba serikali iweze kuingilia kati suala hili ili waweze kupata maji safi na salama kwa wakati muafaka,nawengine wakichukizwa na hali hii nakutaka hata kuondoa mabomba nakuchimba visima ili waweze pata huduma hii ya maji safi na salama kwa uhakika nakuachana na masuala ya mabomba
Aidha wameiomba mamlaka zinazohusika kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu sababu ya kukatika kwa maji na hatua zinazochukuliwa, huku wakitaka huduma hiyo kurejeshwa na kupatikana kwa uhakika.