Mazingira FM

Gari lililobeba mashabiki wa Yanga laua na kujeruhi Bunda

23 July 2023, 8:35 pm

Mashabiki wa club ya Yanga wamesherekea kilele cha siku ya mwananchi kwa masikitiko baada ya miongoni mwa gari lililokuwa limebeba mashabiki wa timu hiyo mjini Bunda kupata ajali iliyosababisha vifo vya watu wawili na kujeruhi wengine 14.

Na Adelinus Banenwa

Watu wawili wamepoteza maisha na wengine 14 kujeruhiwa katika ajali ya gari la mashabiki wa Club ya Yanga wakati wakitoka kuwakarimu wagonjwa hospitali ya Manyamanyama katika siku ya mwananchi.

Tukio hilo limetokea 22 July 2023 hatua chache kutoka viunga vya hospitali ya Manyamanyama baada ya msafara huo wa mashabiki kumaliza kuwasalimia wagonjwa.

Dkt  Deus Nasoro mganga mfawidhi hospitali ya Manyamanyama ameiambia Mazingira FM kuwa hospitali hiyo imepokea miili ya watoto wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 9 hadi 10 na majeruhi 14 waliotokana na ajali hiyo.

Aidha Dkt. Deus amesema majeruhi hao 14 kati yao wana majeraha ya kawaida na wengine wanaendelea na matibabu.

Dkt  Deus Nasoro mganga mfawidhi hospitali ya Manyamanyama

Kwa upande wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema chanzo cha ajali watu kuwa wengi kwenye hilo gari na kuegemea upande mmoja jambo lililopelekea dereva kushindwa kulimudu gario hilo.

Sauti ya shuhuda wa tukio hilo