Mazingira FM

NMB yatoa msaada wa dawati 100 Nyasura

4 October 2023, 3:44 pm

Baadhi ya viongozi wa NMB na serikali wakipeana mikono baada ya kukabidhi Madawati, Picha na Adelinus Banenwa

Katika kuadhimisha wiki ya huduma Kwa wateja banki ya NMB tawi la Bunda wametoa msaada wa madawati 100 kwa sule ya msingi ya Nyasura iliyopo kata ya Nyasura halamshauri ya mji wa Bunda mkoani Mara.

Na Adelinus Banenwa

Katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa mteja banki ya NMB tawi la Bunda wametoa msaada wa madawati 100 kwa sule ya msingi ya Nyasura iliyopo kata ya Nyasura halamshauri ya mji wa Bunda mkoani Mara.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi madawati hayo mkuu wa taasisi za serikali na taasisi binafsi banki ya NMB William Makoresho amesema banki hiyo imekuwa ikishiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kama vile sekta ya elimu, afya na uelimishaji katika mambo mbalimbali.

Amesema katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa mteja wamewiwa kutoa msaada huo kwa shule ya Nyasura kutokana na mahitaji yake ambapo dawati 100 zilizotolewa zimegharimu shilingi 12 milioni.

Mkuu wa taasisi za serikali na taasisi binafsi banki ya NMB William Makoresho, Picha na Adelinus Banenwa
Sauti ya mkuu wa taasisi za serikali na taasisi binafsi banki ya NMB William Makoresho

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Bunda Dr Vicent Anney Naano ameishukuru bank ya NMB kwa kutoa msaada huo huku akibainisha kwa wilaya ya Bunda inaupungufu wa madawati elfu 16  huku halmashauri ya mji wa Bunda ikiwa na upungufu wa madawati elfu 6 .

Mkuu wa wilaya ya Bunda Dr Vicent Anney Naano, Picha na Adelinus Banenwa
Sauti ya mkuu wa wilaya ya Bunda Dr Vicent Anney Naano,

Kwa upande wake mwalimu  mkuu wa shule ya msingi Nyasura mwalimu Benard Ngero Paul  amesema ujio wa madawati hayo kama msaada kutoka NMB  utapunguza changamoto ya uhaba wa madawati japo bado yanaitajika madawati mengi kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi walioko shuleni hapo.

Mwalimu Benard amesema shule ya nyasura ina wanafunzi wapatao 1775 ambapo wasichana ni  985  na wavilana ni 790 ambao wanaitaji madawati 591 huku yaliyopo ni 197 huku upungufu ukitajwa ni madawati 394.

Aidha amebainisha changamoto nyingine ni matundu ya vyoo ambapo kwa mahitaji ni matundu 60 ya vyoo ila yaliyopo ni  12 tu.

Mwalimu  mkuu wa shule ya msingi Nyasura mwalimu Benard Ngero Paul