Mazingira FM

Matumizi yasiyo sahihi ya namba114 changamoto kwa jeshi la Zimamoto Bunda

19 April 2026, 6:23 am

Maafisa kutoka jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Bunda wakiongozwa na mkaguzi msaidizi wa zimamoto na uokoaji DFO Dikson Joseph Madale aliyekaa katikati

Wakati mwingine hupokea simu watu wakitaka kujiunga na freemason, matusi ya nguoni au wakati mwingine habari za uongo kuhusu matukio ya maokozi.

Na Adelinus Banenwa

Imeelezwa kuwa changamoto ya miundombinu, kutotolewa taarifa mapema na taarifa zisizo sahihi bado ni changamoto kwa jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Bunda.

Hayo yameelezwa leo April 18, 2026 na maafisa wa zimamoto na uokoaji kutoka wilaya ya bunda kupitia kipindi cha ufahamu wa sheria kinachorushwa radio mazingira.

Maafisa hao wamesema wakati mwingine hupokea simu watu wakitaka kujiunga na freemason, matusi ya nguoni au wakati mwingine habari za uongo kuhusu matukio ya maokozi hali inayo onekana kama changamoto kwao.

Sauti za maafisa wa zimamoto

Mkaguzi msaidizi wa zimamoto na uokoaji wilaya ya Bunda DFO Dikson Joseph Madale na CPL Magesa Dismas wamesema miongoni mwa majukumu ya zimamoto na uokoaji ni Pamoja na kutoa elimu kwa jamii namna ya kujilinda dhidi ya majanga mbalimbali ikiwemo ajali za moto, kuzama kwenye madimbwi, ziwani au kwenye visima miongoni mwa mengine.

Sauti za maafisa wa zimamoto

Aidha wametoa wito kwa jamii kuzingatia ushauri unaotolewa na maafisa wa zimamoto na uokoaji ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza ikiwemo, watu kuvaa majaketi okozi wakiwa ziwani, kulinda Watoto wasichezee kwenye madimbwi na kutumia namba 114 ili kutoa taarifa za maokozi.