Mazingira FM

Ipi nafasi ya wajane baada ya kupoteza waume zao?

23 June 2025, 5:59 pm

Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda, Salumu Mtelela akikabidhi msaada kwa moja ya wajane

Kwa baadhi ya jamii, wajane hulaumiwa kwa vifo vya waume zao, hutengwa kijamii, na mara nyingine hata kunyimwa urithi au mali walizochuma pamoja.

Na Adelinus Banenwa

Kila mwaka ifikapo tarehe 23 Juni, dunia huadhimisha Siku ya Wajane Duniani (International Widows Day), ikiwa ni fursa ya kuangazia changamoto, uonevu, na unyanyapaa unaowakumba wajane wengi hasa katika nchi zinazoendelea. Siku hii ilianzishwa na Shirika la Umoja wa Mataifa mwaka 2010 kwa kutambua hali ya mateso, umasikini na ukosefu wa haki za msingi kwa wajane duniani kote.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda, Salumu Mtelela akimpakulia chakula moja ya wajane ikiwa ni ishara ya kuonesha dhamani walionayo kwenye jamii

Wajane wengi duniani hupitia kipindi kigumu baada ya kufiwa na waume zao, si tu kiuchungu bali pia kijamii na kiuchumi. Kwa baadhi ya jamii, wajane hulaumiwa kwa vifo vya waume zao, hutengwa kijamii, na mara nyingine hata kunyimwa urithi au mali walizochuma pamoja. Katika baadhi ya mataifa, wajane huishi katika hali duni bila msaada wowote wa kijamii au kisheria.

Kauli mbiu “Innovation and technology for gender equality”yaani

“Ubunifu na teknolojia kwa usawa wa kijinsia.”

Makala nafasi ya wanawake waliopoteza waume zao namna wanavyohangaika kuyakabili maisha