Mazingira FM

Masaburi, vijana changamkia fursa

15 July 2023, 8:47 pm

Mbunge wa viti maalumu kutoka kundi la vijana Mhe Juliana Didas Masaburi akisaini katika kitabu cha wageni katika baraza la UVCCM wilaya aya Bunda, Picha na Adelinus Banenwa

Ili kuhakikisha vijana wanaendelea kujikwamua kimaisha wametakiwa kuchanagmkia fursa zinazotolewa na serikali ikiwa ni pamoja na kuomba mikopo ya asilimia kumi kutoka halmashauri.

Na Adelinus Banenwa

Wito umetolewa kwa vijana mkoani Mara kuchangamkia fursa zinazotolewa na serikali ili kujikwamua kimaisha na kuondokana na utegemezi.
Wito huo umetolewa leo na Mbunge viti maalumu kupitia kundi la vijana Mhe Juliana Didas Masaburi katika baraza la Umoja wa vijana chama cha mapinduzi CCM lililofanyika ukumbi wa Helieth Bunda mjini
Mhe Masaburi amesema badala ya vijana kuangaika kutafuta viongozi kwenye simu ili kupata fursa za ajira au kazi zinanotolewa, wanatakiwa kuziomba fursa hizo kwa wingi ili wachaguliwe

Mhe Juliana Didas Masaburi Mbunge viti maalumu kupitia kundi la vijana

Aidha katika kuwasaidia vijana kuwa na miradi itakayowasaidia kuendesha jumuiya yoa Mhe Juliana amehaidi kuto mashine moja ya kufyatua tofari kwa vijana wa CCM wilaya ya Bunda.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavia Chacha Nyamigeko akiwa mgeni mualikwa katika baraza hilo amesema jumuiya ya umoja wa vijana ina changamoto ya ukosefu wa mradi wa kujiendesha ambpo amesema ili kuondokana na chanagamoto hiyo ameahidi pia kutoa mashine moja ya kufyatua tofari kwa jumuiya hiyo.

Diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavia Chacha Nyamigeko
Diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavia Chacha Nyamigeko

Awali akizungumza katika ufunguzi wa baraza hilo mwenyekiti wa umoja wa vijana chama cha mapinduzi wilaya ya Bunda Mohamed Msafiri amesema kulingana na ukosefu wa chanzo cha mapata katika jumuiya hiyo kinapelekea hata maudhurio katika mabaraza kuwa kidogo

Mwenyekiti UVCCM Bunda Mohamed Msafiri akijadiri jambo na Mhe Mbunge Juliana Masaburi, Picha na Adelinus Banenwa
Mwenyekiti wa umoja wa vijana chama cha mapinduzi wilaya ya Bunda Mohamed Msafiri