Mazingira FM

Mkurugenzi Makumbusho ya Mwalimu Nyerere awapa neno wakazi Kanda ya Ziwa

25 August 2023, 12:25 pm

Emmanuel Kiondo, Mkurugenzi Makumbusho ya Taifa ya Mwalimu Nyerere-Butiama Mkoani Mara akiwa katika studio za Radio Mazingira Fm. Picha na Edward Lucas

Na Edward Lucas

Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa ya Mwalimu Nyerere-Butiama Mkoani Mara, Emmanuel Kiondo awaasa wakazi wa mkoa wa Mara na Kanda ya Ziwa kuwa na tabia ya kutembelea vituo vya utalii

Kiondo ametoa kauli hiyo Agosti 24, 2023 kupitia kipindi cha Meza ya Michezo kinachorushwa na Mazingira Fm wakati alipofika kuhamasisha mbio za Mwl Nyerere Marathon zitakazofanyika mwezi Septemba mwaka huu wilaya ya Butiama.

Amesema kwasasa Makumbusho ya Taifa ya Mwl Nyerere-Butiama yameboreshwa na kuwa ya kisasa zaidi hivyo amewaasa wananchi kutembelea makumbusho hayo kwani kuna mambo mengi ya kujifunza kuhusu historia na urithi wa kihistoria ambao Hayati Mwl Nyerere ameuacha

Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa ya Mwalimu Nyerere Butiama Mkoani Mara, Emmanuel Kiondo