Mazingira FM

TRA: Wafanyabiashara lipeni kodi msisubiri siku ya mwisho kuna faini

21 June 2023, 10:47 am

Afisa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Mamlaka ya Mapato TRA mkoa wa Mara, Geofrey Comoro amewaasa wafanyabiashara wasisubiri siku ya mwisho kufanya malipo ya kodi ya mapato bali wafanye mapema ili kuepuka faini na usumbufu usio wa lazima.

Comoro ameyasema hayo leo tarehe 21 Juni 2023 kupitia mahojiano na Radio Mazingira Fm katika kipindi cha Asubuhi Leo akihamasisha ulipaji wa kodi ya mapato awamu ya pili 2023 na uwasilishaji wa ritani 2022.