Mazingira FM
Mazingira FM
26 April 2026, 12:37 pm

Linapotajwa jambo la dhamani ya fedha kwenye mradi si tu miundombinu imara bali hata miundombinu hiyo kutoa huduma kwa wakati ili malengo ya serikali yaweze kufikiwa.
Na Adelinus Banenwa
Mkuu wa wilaya ya Bunda Mhe Aswege Enock Kaminyoge ametoa siku 14 kwa mkurugenzi wa halamshauri ya mji wa Bunda, afisa elimu wa halmashauri Pamoja na diwani wa kata ya Nyasura kuhakikisha shule ya msingi Victoria inaanza kupokea wanafunzi na wanaanza kusoma.
Shule hiyo iliyo kata ya Nyasura halmasjhauri ya mji wa Bunda mkoani Mara imejengwa kwa lengo la kupunguza mrundikano wa wanafunzi katika shule ya msingi ya Nyasura

Mhe mkuu wa wilaya ametoa maagizo hayo wakati wa zoezi la upandaji miti shuleni hapo katika maadhimisho ya siku ya Muungano yaliyofanyika leo April 26 , 2026 ambapo jumla ya miti 500 imepandwa katika shule hiyo.
Mkuu huyo wa wilaya amesema linapotajwa jambo la dhamani ya fedha kwenye mradi si tu miundombinu imara bali hata miundombinu hiyo kutoa huduma kwa wakati ili malengo ya serikali yaweze kufikiwa.