Mazingira FM
Mazingira FM
8 August 2025, 11:54 am

Msaada huo umetolewa kwa lengo la kuhakikisha watoto hao wanapata huduma za afya kwa urahisi na usalama.
Na Taro Michael
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na waendesha baiskeli wa twende Butiama wametoa msaada wa kadi za bima ya afya kwa wanafunzi wenye uhitaji maalum shule ya msingi Mazoezi.
Katika tukio hilo jumla ya kadi 42 kati ya 80 zenye thamani ya tsh 210,000 Ikiwa na maana kifurushi ni watu sita na Kila kifurushi ni shilingi elfu 30000 zilizolengwa zimekabidhiwa kwa wanafunzi walioainishwa kuwa na uhitaji maalum wa huduma ya afya.

Msaada huo umetolewa kwa lengo la kuhakikisha watoto hao wanapata huduma za afya kwa urahisi na usalama.
Pia Twende Butiama nayo imeungana katika jitihada hizo kwa kutoa viti mwendo 5 pamoja na baiskeli 5 kwa wanafunzi wenye ulemavu, ili kuwawezesha kufika shuleni kwa urahisi zaidi.

Vifaa hivyo vimekabidhiwa rasmi na Bi. Agriphina Mmasi, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi ambaye pia ni msimamizi /kiongozi upande wa wanawake Wilaya ya Bunda.
Akizungumza baada ya kupokea misaada hiyo, Mwalimu Lucy Mlaki kwa niaba ya mkuu wa shule pamoja na wazazi, ameshukuru shukrani Jeshi la Polisi na msafara wa Twende Butiama kwa moyo wa kujitoa kusaidia watoto wenye uhitaji.
Ameeleza kuwa msaada huo ni wa thamani kubwa na umeleta matumaini mapya kwa wanafunzi na familia zao