Mazingira FM
Mazingira FM
14 August 2026, 10:39 am

Mashabiki wa Simba, wamekubali matokeo hayo huku wakitaka viongozi wa klabu hiyo kuboresha kikosi,
Na Juma Hangi
Mashabiki wa Yanga wameeleza furaha yao baada ya timu hiyo kuifunga Simba bao moja kwa sifuri katika mchezo wa Ngao ya Jamii uliochezwa jana, Agosti 12, 2026, katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Mashabiki hao wamepongeza uimara wa kikosi cha Yanga, wakiamini usajili wa wachezaji wapya umeongeza nguvu katika timu hiyo kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kwa upande wa mashabiki wa Simba, wamekubali matokeo hayo huku wakitaka viongozi wa klabu hiyo kuboresha kikosi, hasa safu ya ushambuliaji.
Bao pekee la Yanga lilifungwa dakika ya 31 na mshambuliaji Albert Kangwanda kwa kichwa, na kuifanya Yanga kuibuka na ushindi katika mchezo huo wa ufunguzi wa msimu mpya.
Naye Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amewapa pole mashabiki wa timu hiyo na kuwataka kusahau matokeo hayo na kuelekeza nguvu katika michezo ijayo ya Ligi Kuu Tanzania Bara.