Mazingira FM

Mtoto wa mwaka Mmoja na Nusu apoteza maisha kwa kutumbukia kisimani

3 May 2023, 8:43 am

Kisima alipotumbukia mtoto

Mtoto mmoja Slavic anayekadiriwa kuwa na umri wa mwaka Mmoja na Nusu Mkazi wa Mtaa wa idara ya Maji kata ya Bunda stoo amepoteza maisha kwa kutumbukia kwenye kisima Cha Maji nyumban kwao.

kisima

Tukio hilo limetokea leo asubuhi 2 May 2023 ambopo inaelezwa mtoto huyo alitumbukia kisimani wakati akicheza karibu na hizo kisima jambo lililopelekea kutitia na kusababisha mtoto huyo kutumbukia.

Noela Richard, Shuhuda

Wakizungumza na Mazingira Fm mashuhuda wa tukio hilo Noela Richard amesema kisima hicho kimewekewa mfuniko lakini ndani hakijajengewa hivyo kutokana na mvua inayoendelea kunyesha kimesababisha udongo kuporomoka na kusababisha mtoto huyo kutumbukia.

“Mtoto huyo alikuwa anacheza pembezoni mwa kisima wakati mimi naosha vyombo hapa jirani na mama yake huyo mtoto alikuwa anaosha vyombo nikamwambia kuwa makini na huyo mtoto visima sasa hivi haviaminiki gafla nikaona mama yake Anapiga kelele nami nikashtuka namuuliza nini anasema mtoto katumbukia kwenye kisima huku na yeye akipiga piga miguu akitaka kutumbukia nikaenda haraka nikamvuta kumrudisha nyuma.” Alisema Noela.

Aidha Noela ameongeza kuwa baada kumtoa mama wa mtoto karibu na kisima aliwaita majirani na wapita njia ili kutoa msaada pia aliwapigia viongozi akiwepo Mwenyekiti wa Mtaa pamoja na Diwani Ili kuwapa taarifa juu ya tukio hilo huku jitihada za kumtoa mtoto huyo zikiendelea.

Naye Diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavian Chacha amesema kupitia tukio hilo anawasihi wazazi na walezi kuangalia usalama wa watoto hasa kutocheza karibu na maeneo hatarishi hasa visimani na maeneo mengine kama hayo.

Aidha amewaagiza wenyeviti wa mitaa, na watendaji kuhakikisha wanapita kwenye maeneo yao yote kuona ubora wa visima na mashimo ya vyoo na kuona namna ya kuwasaidia wananchi hao.