Mazingira FM

RC Mara: Walimu zingatieni sheria sasa hivi dunia ni ya utandawazi

27 July 2023, 8:25 pm

Mkuu wa mkoa wa Mara Said Mohamed Mtanda katika ziara wilayani Bunda, Picha na Thomas Masalu

Walimu zingatieni sheria kwa sasa dunia ni ya utandawazi watu wanarekodi kila kitu na kutuma kwenye mitandao.

Na Thomas Masalu

Mkuu wa mkoa wa Mara, Mhe Said  Mohamed  Mtanda amewataka walimu kuzingatia sheria katika utekelezaji wao wa majukumu ili kuondoa migongano na jamii inayowazunguka.

Mhe  Mtanda ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na walimu wa shule ya  msingi Miembeni A mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja na matundu ya vyoo katika shule hiyo, ujenzi huo unatekelezwa kupitia mradi wa BOOST.

Aidha Mhe Mtanda amesema siku hizi mambo mengi yamekuwa wazi na watu wana rekodi kila kitu na kurusha kwenye mitandao hivyo walimu wana jukumu la kufanya kazi yao kwa weledi mkubwa.

Sauti ya Rc Mara Said Mohamed Mtanda
Mkuu wa mkoa wa Mara Said Mohamed Mtanda katika ziara wilayani Bunda, Picha na Thomas Masalu

Katika hatua nyingine  Mtanda, akiwa shule ya msingi Mazoezi amewakumbusha wanafunzi kuacha mara moja tabia ya kupokea zawadi njiani maana siku hizi matukio ya ukatili yamekuwa mengi kwa watoto.

Ameongeza kuwa  wanafunzi wanapaswa kutoa taarifa kwa mwalimu mkuu pale wanapoona dalili ya kutaka kufanyiwa ukatili ili hatua zichukuliwe dhidi ya yule anayetaka kufanya tukio hilo.

Sauti ya Rc Mara Said Mohamed Mtanda