Mazingira FM

Nyamoko yaaga changamoto ya mawasiliano Yas ikizindua mnara

24 July 2026, 10:18 pm

Diwani wa kata ya Nyamoko Mhe Emmanuel Gabriel Saina

Mwanzoni ilikuwa changamoto katika vijiji vya kata hiyo kwenye suala la mawasiliano hali iliyokuwa inapelekea Kwenda mbali kutafuta mawasiliano

Na Adelinus Banenwa

Diwani wa kata ya Nyamoko iliyopo wilayani Serengeti mkoani Mara Mhe Emmanuel Gabriel Saina ameupongeza mtandao wa simu wa YAS kwa kuzindua mnara ambao utasaidia kutatua changamoto ya mawasiliano kwenye kata hiyo na vijiji Jirani.

Akiwa mgeni rasmi Mhe Saina ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa mnara wa YAS uliopo Kijiji cha Itununu wilayani Serengeti ambapo amesema mwanzoni ilikuwa changamoto katika vijiji vya kata hiyo kwenye suala la mawasiliano hali iliyokuwa inapelekea Kwenda mbali kutafuta mawasiliano

Amesema uwepo wa huduma hiyo kwa sasa itasaidia pia vijana kujiajili mfano kufungua za kifedha kama MIXX  BY YAS Pamoja na kusajili line.

Meneja wa YAS Mara ya kusini Ndugu Kharid Omary Mtwange
Sauti ya Mhe Emmanuel Gabriel Saina

Kwa upande wake meneja wa YAS Mara ya kusini Ndugu Kharid Omary Mtwange amesema baada ya kupokea maombi kutoka kwa wakazi wa maeneo hayo na wao kama mtandao walifanya utafiti leo wamezindua mnara huo ambao anaamini utawasaidia wananchi ambao wamekuwa wakipata changamoto ya mawasiliano na yas wamekuwa wakifanya hivyo kwa maeneo yote nchini ili kuahkikisha hakuna mwananchi anakosa mawasiliano.

Sauti ya Kharid Omary Mtwange
Timu ya wafanyakazi wa YAS wakifurahia baada ya kuzindua mnara kijiji cha Itununu kata ya Nyamoko

Awali badhi ya wakazi wa kitongoji cha Itununu ameushukuru mtandao wa YAS  kwa kuwasogezea huduma hiyo karibu kwa kuwa wamekuwa wakipata changamoto ya mawasiliano huku wakihamasisha wananchi wengine ambao hawana line kuhakikisha wanazipata .