Mazingira FM

Mikakati kupambana na wanyama waharibifu yawekwa wazi Bunda

21 July 2023, 9:12 pm

Dr Vicent Naano Anney, Mkuu wa Wilaya ya Bunda akizungumza na wananchi kijiji cha Sarakwa. Picha na Edward Lucas

Kuongeza magari, kuweka uzio wa waya na kuongeza vituo vya vikosi vya kudhibiti wanyamapori waharibifu ni miongoni mwa mikakati iliyojadiliwa katika kusaidia kilio cha wananchi wanaopakana na hifadhi ya Serengeti jimbo la Bunda.

Na Edward Lucas

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Dr. Vicent Naano ameahidi kusimamia upatikanaji wa magari mawili ili kusaidia juhudi za kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu.

Dr Naano amebainisha hayo kupitia mkutano ulioratibiwa na mbunge wa jimbo la Bunda mheshimiwa Boniphace Mwita Getere ukiwakutanisha wananchi, viongozi na taasisi za uhifadhi pamoja na wadau wa uhifadhi ili kujadili mikakati ya kukabiliana na wanyama hao.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dr. Vicent Naano kuhusu mkakati wa kuongeza magari

Akizungumzia mkakati huo, Kamishna Msaidizi TAWA, Said Kabanda amesema jambo la kukabiliana na wanyamapori waharibifu linahitaji ushirikiano wa wadau wote wakiwemo wananchi na taasisi zingine ili kufanikisha zoezi 

Kamishna Msaidizi TAWA, Said Kabanda katika viwanja vya shule ya msingi Stephen Wasira kijiji cha Sarakwa akizungumza na wananchi kuhusu mikakati kukabiliana na wanyama waharibifu
Sauti ya Kamishna Msaidizi TAWA, Said Kabanda akiweka bayana mikakati

Kwa upande wake Mbunge Boniphace Getere amezitaka mamlaka na taasisi husika kuangalia uwezekano wa kuweka uzio wa waya kama wananchi walivyoomba.

Mbunge Boniphace Mwita Getere akisisitiza kwa mamalaka mpango wa waya kuzuia wanya waharibifu
Maoni ya wananchi kuhusu adha wanayoipata kwa wanyama waharibifu