Mazingira FM

Mifugo na tabia ya nchi changamoto kwa mazingira

3 June 2026, 7:13 pm

Mkurugenzi wa BUFADESO Baraka Kamese

Aidha Baraka amesema  changamoto ya mabadiliko ya tabia ya nchi ikiwemo vipindi virefu vya jua na mvua vinasababisha uharibifu wa mazingira.

Na Adelinus Banenwa

Mifugo, mabadiliko ya tabia ya nchi na upungufu wa rasilimali  bado ni changamoto kubwa katika kampeni ya utunzaji wa mazingira

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa BUFADESO Baraka Kamese kupitia Mazingira FM kwenye kipindi cha kilimo na mifugo ambapo ameeleza kuwa mara nyingi wao kama BUFADESO wamekuwa wakitoa miti kwa taasisi mbalimbali lakini changamoto kubwa imekuwa ni wachungaji wa mifugo kupeleka mifugo yao kwenye maeneo ya ambayo miti imepandwa

Aidha Baraka amesema  changamoto ya mabadiliko ya tabia ya nchi ikiwemo vipindi virefu vya jua na mvua vinasababisha uharibifu wa mazingira .

Sauti ya Mkurugenzi wa BUFADESO Baraka Kamese

Amesema kutokana ana hayo BUFADESO wameendelea kutoa elimu katika vikundi mbalimbali vya wakulima ikiwemo kushirikiana na serikali za halmashauri kupanda miti katika maeneo ya taasisi.