Mazingira FM

Bunda: Mwili mmoja wapatikana kati ya 13 wanaoohofiwa kufa maji Ziwa Victoria

1 August 2023, 5:04 pm

Wananchi wakiwa kandokando ya Ziwa Victoria eneo la Mchigondo Bunda wakiendelea kufuatilia zoezi la utafutaji waliozama. Picha na Adelinus Banenwa

Mwili mmoja umepatikana leo majira ya saa saba mchana katika zoezi la kuwatafuta watu 13 waliozama Ziwa Victoria kijiji cha Mchigondo kata ya Igundu Wilaya ya Bunda.

Na Edward Lucas

Mwili mmoja wapatikana kati ya 13 wanaoohofiwa kufa maji ziwa Victoria katika ajali ya mitumbwi kijiji Mchigondo Bunda na kufanya idadi ya waliofariki kufikia watu 2 mpaka sasa huku zoezi la kuwatafuta wengine 12 likiwa linaendelea.

Aliyepatikana leo majira ya saa saba mchana ni Pendo Charles (13) mkazi wa Sunsi mwanafunzi wa darasa la 7 shule ya Msingi Bulomba ambaye tayari mwili wake umekabidhiwa kwa familia kwa ajili ya kuendelea na shughuli za mazishi.

Akizungumzia zoezi hilo, Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara, Agostino Magere amesema juhudi za kuwatafuta wengine bado zinaendelea licha ya kukutana na changamoto kadhaa katika zoezi hilo.

Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara, Agostino Magere