Mazingira FM

Halmashauri ya Mji wa Bunda yapokea tani 30 za mahindi ya bei nafuu

13 September 2022, 7:49 am

Halmashauri ya Mji wa Bunda imepokea tani 30 za mahindi ya bei nafuu kutoka kwa wakala wa hifadhi ya chakula ya Taifa NFRA

 

Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake Katibu tawala Wilaya ya Bunda Salum halfani Mterela amesema mahindi yaliyoletwa ni kwa ajili ya wananchi wa kawaida kwa ajili ya chakula

 

Mterela ametoa ufafanuzi kuwa kilo Moja ya mahindi itauzwa kwa shilingi 920 huku akisisitiza kuwa mwananchi anayetaka kununua kuanzia gunia Moja yaaani kilo 100 anatakiwa awe na uthibitisho wa barua ya afisa mtendaji

 

Aidha ametoa onyo Kali kwa wafanyabiashara kutojiingiza kwenye ununuzi wa mahindi hayo kwa namna yoyote kwa kuwa mbinu zote wanazozitumia wameishazibaini hivyo wazingatie kwamba mahindi haya ni kwa ajili ya chakula kwa wananchi

 

Ametoa Rai kwa wananchi kutokubali kutumiwa na wafanyabiashara ili lengo la serikali liweze kufikiwa

 

Mterela amesema mahindi hayo yanapatika katika stoo ya Bunda mjini iliyopo karibu na shule ya msingi Miembeni