Mazingira FM

Mwenge wa uhuru wateketeza zana haramu za uvuvi Bunda

13 July 2023, 9:49 am

Zana haramu za uvuvi zilizoteketezwa na kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa 2023 Ndgu Abdallah Shaibu Kaim eneo la Mwalo wa Kibra Bunda. Picha na Thomas Masalu

Mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2023 katika halmashauri ya wilaya Bunda imetembelewa miradi 7 ambapo miongoni mwa shughuli zilizofanyika ni uteketezaji wa zana haramu za uvuvi ikiwa ni jitihada za kulinda na kutunza mazingira.

Na Thomas Masalu

Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa 2023 ameteketeza zana haramu za uvuvi zilizokamatwa hivi karibu na maafisa wa uvuvi wa Halmashauri hiyo katika mwalo wa Kibara Kata ya Kibara halmashauri ya wilaya ya Bunda.

Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa 2023 Ndgu Abdallah Shaibu Kaim, kulia na mkuu wa wilaya ya Bunda Mhe Dkt Vicent Anney Naano, katika moja ya mradi wa utunzaji wa mazingira uliozinduliwa na mwenge katika halimashauri ya wilaya ya Bunda, Picha na Thomas Masalu

Akiteketeza zana hizo, Abdalah Shaibu Kaim amesema serikali haiwezi kufumbia macho uvuvi haramu hivyo ni vyema wananchi wakaachana na shughuli ya uvuvi haramu maana hailipi.

Abdalah Shaibu Kaim Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa 2023

Aidha amewaomba wananchi kuendelea kuwa mabalozi wema katika utuzanji wa rasiliamali ili kizazi kijacho kifaidike na rasiliamali zilizopo.

Uteketezaji huo umefanyika leo katika eneo la mwalo wa Kibara ambapo pia choo cha matundu matano chenye lengo la uboreshaji wa mazingira kimezinduliwa.

Hiyo ikiwa ni miongoni mwa miradi kati ya miradi 7 iliyotembelewa na mwenge wa uhuru 2023 ndani ya halmashauri ya wilaya ya Bunda.