Mazingira FM

Diwani Flaviani aaga WDC Bunda stoo, wajumbe wampongeza kwa miradi

11 June 2025, 11:27 am

Diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavian Chacha Nyamageko

Kiasi cha shilingi bilion 5.71  kimetolewa na serikali kwa ajili ya utekelezaji wa  shughuli za maendeleo kwa kata ya Bunda stoo katika kipindi cha miaka mitano yaani 2021 na 2025.

Na Adelinus Banenwa

Kiasi cha shilingi bilion tano milioni miasaba na kumi lakisaba na hasini na nane miatatu arobaini na moja  (5,710,758,341) kimetolewa na serikali kwa ajili ya utekelezaji wa  shughuli za maendeleo kwa kata ya Bunda stoo katika kipindi cha miaka mitano yaani 2021 na 2025.

Hayo yamebainishwa Jumanne june 10 , 2025 kupitia taarifa ya diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavian Chacha Nyamageko mbele ya wajumbe wa baraza la maendeleo la kata ya Bunda stoo lililoketi ambapo pamoja na mambo mengine baraza hilo lilikuwa na kazi ya kumuaga diwani huyo baada ya kufanya naye kazi katika kipindi ambacho yeye alikuwa diwani na mwenyekiti wa baraza.

Diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavian Chacha Nyamageko ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la maendeleo la kata ya Bunda stoo akilishwa keki na mtendaji wa kata hiyo ambaye pia ni katibu wa baraza la WDC

Akisoma taarifa mbele ya wajumbe wa baraza la maendeleo la kata kwa niaba ya diwani,  mwenyekiti wa mtaa wa Butakare Sebastian Chacha Masugo amesema fedha hizo zimefanikisha kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo miradi ya Afya , Maji, Elimu, Barabara, Umeme miongoni mwa miradi mingine.

Sauti ya mwenyekiti wa mtaa wa Butakare Sebastian Chacha Masugo
Diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavian Chacha Nyamageko akipokea zawadi ya kiatu kutoka kwa wajumbe wa Baraza la maendeleo la kata

Kwa upande wake diwani wa kata hiyo Mhe Flavian Chacha amelishukuru baraza hilo kwa moyo wa upendo waliouonesha kwake katika kipindi chote ambacho amefanya nao kazi, huku akitambua mchango wao kama wajumbe kwa juhudi walizofanya kuwezesha fedha zilizoletwa na serikali zinatekeleza miradi husika kwa maslahi ya wananchi.

Sauti ya Diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavian Chacha Nyamageko

Baraza hilo kwa kutambua mchango wa diwani huyo pia walitoa zawadi mbalimbali kwa mwenyekiti wao huku Mhe Nyamigeko akitamka wazi kuwa baada ya baraza la madiwani kuvunjwa atakwenda kuchukua fomu kutetea nafasi yake,