Mazingira FM

Bunda: Miili yote 13 yapatikana ajali ya mitumbwi Ziwa Victoria

2 August 2023, 9:55 pm

Kandakando ya Ziwa Victoria eneo la Mchigondo Wilaya ya Bunda katika zoezi la utafutaji waliopata ajali ya mitumbwi miwili. Picha na Adelinus Banenwa

28 walipata ajali 30 July 2023, wakanusurika 14 siku ya tukio , mtoto wa mwaka mmoja akapatikana akiwa amefariki na katika zoezi la utafutaji tarehe 1 August 2023 hadi kufikia saa 12:00 jioni wawili walikuwa wamepatikana na kufika asubuhi 2 August 2023 miili 10 ikawa imepatikana na majira ya saa 6:00 mchana mwili wa mwisho ukapatikana idadi imekamilika 28 zoezi limefungwa.

Na Thomas Masalu

Shughuli ya uokozi katika ajali ya mitumbwi miwili iliyozama ndani ya Ziwa Victoria na kusababisha vifo vya watu 14 wilayani Bunda imekamilika baada ya miili yote kuopolewa.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara,  Agostino Magere amesema kazi hiyo imekamilika baada ya mwili wa 13 kuopolewa baada ya takriban siku nne za uokozi.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara,  Agostino Magere

Aidha Magere amebainisha changamoto walizokutana nazo katika utekelezaji wa shughuli hiyo ya uokozi.

Naye kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Mara mheshimiwa Said Mtanda amesema kuwa Rais Dkt .Samia Suluhu ametuma salam za pole kwa wananchi wa mkoa wa Mara kufuatia ajali hiyo.